Shirika la habari la ABNA linaripoti kuwa: Korea kaskazini leo imefanikiwa kufanya jaribio la kombora kutoka katika meli ya kijeshi. kombora hilo liliangukia katika bahari ya Japan.
Ni jaribio la hivi karibuni kabisa miongoni mwa majaribio kadhaa yaliyofanywa na nchi hiyo ikikaidi maazimio ya baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Waziri wa mambo ya kigeni wa Japan Fumio Kishida amesema jumuiya ya kimataifa inapaswa kuchukua hatua.
Jaribio hilo lilifanyika siku mbili tu baada ya Korea kusini na Marekani kuanza luteka yao ya kijeshi ya kila mwaka nchini Korea kusini, ambayo Korea ya kaskazini inashutumu hatua hiyo.
Marekani imekuwa ikitumia ushawishi wake kuikandamiza nchi hiyo iliyopinga kabisa kuwa chini ya amri za Marekani .
Mwisho wa habari/ 291